by Rev. Dr. Allen Adam Mbiso
Nguvu ya Maagano Saba ya Mungu ni mwongozo wa kibiblia unaofunua maagano ya Adamu, Nuhu, Ibrahimu, Musa, Daudi, Agano Jipya na Agano la Milele, na jinsi yote yanavyodhihirisha upendo, neema, ukombozi na kusudi la Mungu kwa mwanadamu. Kitabu kinaeleza ahadi, masharti, damu na muhuri wa kila agano, huku kikimwonesha msomaji jinsi yanavyotimia katika Yesu Kristo. Kwa kukisoma, utaimarisha imani yako katika ahadi za Mungu, kupata ujasiri katika maombi na kuelewa ushindi uliopo katika damu ya Yesu dhidi ya hofu na maagano ya giza. Hii ni eBook muhimu kwa Mkristo anayetafuta ufahamu wa kina, uhakika wa wokovu na maisha ya ushindi. Wasiliana na Mwandishi kupitia: